Somo la Kwanza: Kut 17:8-13
Somo la Pili: 2 Tim 3:14-4:2
Injili: Lk 18:1-8
Somo la Kwanza: Kut 17:8-13
Somo la Pili: 2 Tim 3:14-4:2
Injili: Lk 18:1-8
Utangulizi: Ndugu zangu wapendwa leo tunakumbushwa kuomba bila kuchoka. Sala ni kumuinulia Mungu mioyo na akili zetu. Moja kati ya namna ya kusali leo ni udumivu katika sala. Kuomba bila kuchoka; tunapata fundisho hilo katika somo la 1 na Injili. Na katika somo la II, tunaambiwa tunachota sala katika neno la Mungu.
HOMILIA
Sala sio kitu kigeni katika maisha yetu ya ufuasi, katika maisha yetu ya imani. Ni wazi kuwa imani yetu tumeijifunza tokea tukiwa wadogo kwa kusali. Na tunaendelea kusali. Na hata tendo tunalofanya la sadaka ya Misa ni sala, tena kilele cha sala zote, kwani tunaweza kuzungumza na Yesu moja kwa mmoja katika Ekaristi takatifu, tunagusa huruma yake kwa mioyo, akili, mikono, na vinywa vyetu.
Somo la I: Katika somo la kwanza tunaona nguvu ya Mungu katika sala. Tunaona Waisrael wanapambana na Waameleki Jangwani. Musa akiwa juu ya Mlima. Anainua mikono yake juu na wakati ameinua mikono, Waisrael wanashinda. Anaposhusha tu wanapigwa. Kuinua mikono ni ishara ya sala.
Ndugu wapendwa tunaona umuhimu wa sala katika maisha yetu ya imani. Tunaposali, adui anashindwa. Tunapoacha kusali adui anashinda. Inua Mikono yako ushinde.
Lakini pia tunaona Musa anasali sio kwa ajili yake, bali kwa ajili ya watu wengine. Usichoke kuinua mikono yako juu ya familia yako, juu ya mume wako, juu ya mke wako, juu ya jamaa zako, juu ya wazazi wako, na hata juu ya adui zako. Unaposhusha mikono yako, yaani unapoacha kusali, kuna watu wanateseka.
Somo la II: Tunapokuwa tunakosa nguvu ya sala, basi tumepewa pa kuchota nguvu. Tumepewa maandiko matakatifu. Yaani Neno la Mungu. Paulo anasema lina nguvu. Linatuhekimisha, limejaa hekima. Na linafaa kwa kuwaonya watu makosa yao. Hivyo tuikimbilie biblia tulisome Neno, ni taa ya kutuongoza katika sala. Linatupa nguvu ya kuwa watu wa sala bila kuchoka na pia kuwa wamisionari kweli. Hapa tutamkumbuka mt. Jerome na fundisho lake; “Ignorance of the Scripture is ignorance of Christ.” Yaan kutokujua maandiko ni kutokumjua Yesu.
Injili: Katika somo la Injili, Yesu anakazia kuhusu Udumivu katika sala kwa mfano wa mama mjane aliyekwenda mara kwa mara kwa hakimu dhalimu, akimwomba atende haki. Hatimaye hakimu alikubali ombi lake si kwa sababu alikuwa mwema, tunaambiwa alikuwa dhalimu, bali ni kwa sababu ya udumivu, na uvumilivu wa yule mjane.
Ndugu zangu Mungu hutenda haki kwa wakati wake: Injili inatuambia Mungu yuko mbali sana, hawezi kulinganishwa na yule hakimu dhalimu. Cha msingi tusali bila kukata tamaa. Endelea kuomba bado kitambo kidogo utafanikiwa.
Imani ya kweli huonekana katika matendo ya kudumu: mjane yule alisisitiza kuiendea haki yake kwa hakimu. Hii inatukumusha pia kwamba matendo yetu yanatakiwa kuakisiwe katika sala na imani.
Zifuatazo ni baadhi ya sifa za sala ya kiimani